Amezaliwa | 2 Januari 1968 Dar es Salaam |
---|---|
Nchi | Tanzania |
Kazi yake | Mtaalamu wa mazingira |
Joyce Msuya (alizaliwa Dar es Salaam, 2 Januari 1968) ni mwanabiolojia na mtaalamu wa mazingira kutoka Tanzania, aliyekuwa Katibu Mkuu Msaidizi wa UM kwa Shughuli ya Hisani na mratibu msaidizi wa miradi ya misaada ya hisani ya Umoja wa Mataifa.[1].
Hadi kuteuliwa kwa kazi hiyo Desemba 2021 alikuwa Kaimu Mkurugenzi Tekelezi wa Mradi wa Umoja wa Mataifa Kuhusu Mazingira (UNEP) na Msaidizi wa Katibu Mkuu wa UM tangu mwaka 2018.[2].